Mwimbaji tegemeo wa Jahazi Modern Taarab, Mishi Zele (pichani juu) amewaacha njia
panda mashabiki wake baada ya hatma yake kuning’inia baina ya bendi mbili
pinzani.
panda mashabiki wake baada ya hatma yake kuning’inia baina ya bendi mbili
pinzani.
Msanii huyo anayetesa na wimbo wake “Nia Safi Hairogwi” kwasasa
anahusishwa kwa nguvu na uhamisho wa kwenda Yah TMK Modern Taarab.
anahusishwa kwa nguvu na uhamisho wa kwenda Yah TMK Modern Taarab.
Kwa wiki mbili sasa, Mishi haonekani kwenye jukwaa la Jahazi na badala
yake amekuwa akishiriki maonyesho ya kundi la Yah TMK Modern Taarab.
yake amekuwa akishiriki maonyesho ya kundi la Yah TMK Modern Taarab.
Hapo kabla, Saluti5 ilielezwa kuwa Mishi ni miongoni mwa waimbaji
watano waliogoma kazi kwa madai ya kutolipwa stahiki zao.
watano waliogoma kazi kwa madai ya kutolipwa stahiki zao.
Waimbaji wengine wanaotajwa katika mpango huo ni Hadija Mbegu, Marim
Kasola, Mariam BSS na Mwanaidi Ramadhani.
Kasola, Mariam BSS na Mwanaidi Ramadhani.
Wakati waimbaji hao wengine bado hawajaanza kuhusishwa na uhamisho wa
kwenda bendi nyingine, Mishi ana anahusishwa sana na Yah TMK.
kwenda bendi nyingine, Mishi ana anahusishwa sana na Yah TMK.
Saluti5 ilipomuuliza Mishi juu ya uvumi huo wa kujiunga na Yah TMK,
hakukanusha waka kukubali.
hakukanusha waka kukubali.
Mishi alisema: “Mimi nina madai yangu Jahazi ambayo kwasasa sina haja
ya kuyaweka wazi. Yah TMK ni bendi kubwa na inanivutia kufanya nayo kazi.
ya kuyaweka wazi. Yah TMK ni bendi kubwa na inanivutia kufanya nayo kazi.
“Kama nitaondoka Jahazi basi sitakuwa msanii wa kwanza kufanya hivyo
wala sitakuwa wa mwisho. Jahazi ni bendi yangu na ninaipenda lakini maisha
popote. Baada ya wiki mbili nitaweka wazi hatma yangu”.
wala sitakuwa wa mwisho. Jahazi ni bendi yangu na ninaipenda lakini maisha
popote. Baada ya wiki mbili nitaweka wazi hatma yangu”.
Kuhusu kuonekana kwenye jukaa la Yah TMK, Mishi alisema bendi ile ni
kama nyumbani kwake kwa vile ina wasanii wengi aliofanya nao kazi Jahazi.
kama nyumbani kwake kwa vile ina wasanii wengi aliofanya nao kazi Jahazi.
Uongozi wa Jahazi umeiambia Saluti5 kuwa wasanii hao watano wametakiwa
kuandika barua ya kuomba radhi kabla ya kurejeshwa kazini, lakini habari za
ndani kabisa zinadai kuwa kuna wasanii ambao hawako tayari kuomba radhi huku
wengine wakiwa mbioni kuandika barua ya kukiri makosa.
kuandika barua ya kuomba radhi kabla ya kurejeshwa kazini, lakini habari za
ndani kabisa zinadai kuwa kuna wasanii ambao hawako tayari kuomba radhi huku
wengine wakiwa mbioni kuandika barua ya kukiri makosa.